Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Yanga wazindua jezi mpya 2020/21
Michezo

Yanga wazindua jezi mpya 2020/21

Spread the love

MABINGWA wa kihistoria wa soka nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam, wamezindua jezi mpya ambazo zitatumika katika msimu wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwapungu, Dar es Salaam … (endelea).

Uzinduzi huo umefanyikia makao makuu ya timu hiyo, Jangwani leo Ijumaa tarehe 11 Septemba, 2020 na kuhudhuriwa viongozi mbalimbali wa Yanga akiwemo Makamu Mwenyekiti wake, Fredrick Mwakalebela na Mshauri wa timu hiyo, Senzo Mazingisa.

Yanga imekuwa klabu ya kwanza Tanzania kuwa na duka lake la vifaa vya michezo katika makao ya timu ambapo, Senzo amewaomba mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kununua ili kuongeza mapato ya timu na kuifanya kuendelea kuwa bora zaidi ndani na nje ya Tanzania.

Senzo amesema huo ni mwelekeo mzuri wa timu kuwa na duka lake la vifaa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa GSM, Hersi Said amesema, kila mwaka watakuwa wanatengeneza jezi nzuri “hatutengenezi jezi tu bora tumetengeneza” na zitakuwa zinaendena na tamaduni za Kiafrika na ki-Yanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!