Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga wazindua jezi mpya 2020/21
Michezo

Yanga wazindua jezi mpya 2020/21

Spread the love

MABINGWA wa kihistoria wa soka nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam, wamezindua jezi mpya ambazo zitatumika katika msimu wa 2020/21. Anaripoti Kelvin Mwapungu, Dar es Salaam … (endelea).

Uzinduzi huo umefanyikia makao makuu ya timu hiyo, Jangwani leo Ijumaa tarehe 11 Septemba, 2020 na kuhudhuriwa viongozi mbalimbali wa Yanga akiwemo Makamu Mwenyekiti wake, Fredrick Mwakalebela na Mshauri wa timu hiyo, Senzo Mazingisa.

Yanga imekuwa klabu ya kwanza Tanzania kuwa na duka lake la vifaa vya michezo katika makao ya timu ambapo, Senzo amewaomba mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kununua ili kuongeza mapato ya timu na kuifanya kuendelea kuwa bora zaidi ndani na nje ya Tanzania.

Senzo amesema huo ni mwelekeo mzuri wa timu kuwa na duka lake la vifaa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa GSM, Hersi Said amesema, kila mwaka watakuwa wanatengeneza jezi nzuri “hatutengenezi jezi tu bora tumetengeneza” na zitakuwa zinaendena na tamaduni za Kiafrika na ki-Yanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!