Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Pogba aambukizwa corona, atoswa Ufaransa
KimataifaMichezo

Pogba aambukizwa corona, atoswa Ufaransa

Paul Pogba
Spread the love

PAUL Pogba, kiungo wa Manchester United, ameachwa katika kikosi cha Timu ya Taifa ya Ufaransa, baada ya kubainika kuambukizwa virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea)

Kikosi hicho cha Ufaransa kitacheza michezo miwili ya kirafiki na Sweden tarehe 5 Septemba 2020 na mchezo wa pili kitacheza nyumbani Paris 8 Septemba 2020.

Mchezaji mwingine ambaye ameachwa katika kikosi hicho baada ya kukutwa na  corona ni kiungo wa Tanguy Ndombele wa timu ya Tottenham Hotspur ya Uingereza.

Kocha wa timu hiyo, Didier Deschamps amesema, ameamua kufanya mabadiliko ya kumwita kikosini Eduardo Camavinga wa timu ya Rennes ya Ufaransa kuchukua nafasi ya Pogba ambaye jana alipimwa na kukutwa na corona.

Paul Pogba

Wawili hao wamelazimika kusalia Uingereza kwa mujibu wa taratibu, wanapaswa kujitenga kwa siku 14.

Hatua hiyo, inawafanya wachezaji hao kila mmoja kukosa maandalizi ya msimu wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) itakayoanza tarehe 12 Septemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!