RAIS John Magufuli ameshauri Kanisa la Assembly of God (TAG), kuelekenza nguvu katika ujenzi wa viwanda. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Ametoa kauli hiyo jijini Dodoma leo tarehe 14 Agosti 2020, wakati wa Maadhimisho ya Miaka 13 ya Moto katika Mkutano Mkuu wa kanisa hilo.
Ni baada ya kanisa hilo kueleza, kwamba limetenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu.
“Nataka nikuhakikishie Askofu Mkuu tuko pamoja katika hilo, na mimi nafikiri sio tu kujenga Chuo Kikuu lakini mnaweza kutenga eneo kwa ajili ya kujenga viwanda.
“Hata kama ungeanzisha kiwanda cha kuchimba chuma kule Manda ili sisi Tanzania tusiwe tunaagiza chuma kutoka kule nje. Tuchimbe chuma yetu ambayo ni first class (Daraja la Kwanza)..halafu na madini mbalimbali na viwanda vile vikawa chini ya TAG,” amesema Rais Magufuli.
Amesema, nafasi ya kuanzisha viwanda katika serikali yake bado hipo “kwa hiyo Baba Askofu Mkuu na ndugu wachungaji na maaskofu wote, chumba hicho bado kipo wazi.
“…na mimi napenda kuwathibitishia kabisa kwasababu tunaijenga Tanzania ya viwanda, mimi na serikali yangu kama tupo, tutaendelea kuwasapoti kwa nguvu zote.”
Leave a comment