Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: TAG jiengeni viwanda
Habari za Siasa

Rais Magufuli: TAG jiengeni viwanda

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ameshauri Kanisa la Assembly of God (TAG), kuelekenza nguvu katika ujenzi wa viwanda. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo jijini Dodoma leo tarehe 14 Agosti 2020, wakati wa Maadhimisho ya Miaka 13 ya Moto katika Mkutano Mkuu wa kanisa hilo.

Ni baada ya kanisa hilo kueleza, kwamba limetenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu.

“Nataka nikuhakikishie Askofu Mkuu tuko pamoja katika hilo, na mimi nafikiri sio tu kujenga Chuo Kikuu lakini mnaweza kutenga eneo kwa ajili ya kujenga viwanda.

“Hata kama ungeanzisha kiwanda cha kuchimba chuma kule Manda ili sisi Tanzania tusiwe tunaagiza chuma kutoka kule nje. Tuchimbe chuma yetu ambayo ni first class (Daraja la Kwanza)..halafu na madini mbalimbali na viwanda vile vikawa chini ya TAG,” amesema Rais Magufuli.

Amesema, nafasi ya kuanzisha viwanda katika serikali yake bado hipo “kwa hiyo Baba Askofu Mkuu na ndugu wachungaji na maaskofu wote, chumba hicho bado kipo wazi.

“…na mimi napenda kuwathibitishia kabisa kwasababu tunaijenga Tanzania ya viwanda, mimi na serikali yangu kama tupo, tutaendelea kuwasapoti kwa nguvu zote.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!