Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wiki hii: JPM, Lissu ‘kukutana’ NEC
Habari za SiasaTangulizi

Wiki hii: JPM, Lissu ‘kukutana’ NEC

Spread the love

MIOAMBA miwili ya siasa nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020, inatarajiwa ‘kupigana kumbo’ katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi (NEC), Dodoma wakati wa kuchukua fomu za urais. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wakati Tundu Lissu, mgombea urais wa Chama cha Demkrasia na Maendeleo (Chadema), akitangazwa kuchukua fomu ya kugombea urais wiki hii tarehe 8 Agosti 2020, Dk. John Magufuli ndani ya waki hii atachukua fomu.

Mpaka leo, zimebaki siku tano kukamilika wiki ambapo kila mmoja anatarajiwa kufika kwenye ofisi hizo zinazotumia majengo yake mapya yaliyopo katika eneo la Njendengwa, jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo tarehe 5 Agosti 2020, mbele ya waandishi wa jijini Dar es Salaam, Dk. Magufuli ambaye ni Rais wa sasa wa Tanzania, atafika kwenye ofisi za NEC kuchukua fomu ya kugombea urais, hata hivyo hajataja siku, tarehe wala muda wa tukio hilo.

            Soma zaidi:-

 

“Napenda kuwatangazia rasmi kabisa, mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ambaye sisi kwenye chama chetu ndio muasisi mkubwa wa uwazi, atachukua fomu wiki hii, ni lini nitawaambia tena, lakini wiki hii mgombea CCM atachukua fomu kule jijini Dodoma,” amesema Polepole.

Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020, ambapo NEC imefungua zoezi la uchukuaji fomu ngazi ya urais kuanzia leo na kuhitimishwa tarehe 25 Agosti mwaka huu.

Rais Magufuli alipitishwa na Mkutano Mkuu wa CCM kugombea nafasi hiyo Julai mwaka huu. Rais Magufuli anagombea kwa mara ya pili baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!