Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wiki hii: JPM, Lissu ‘kukutana’ NEC
Habari za SiasaTangulizi

Wiki hii: JPM, Lissu ‘kukutana’ NEC

Spread the love

MIOAMBA miwili ya siasa nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020, inatarajiwa ‘kupigana kumbo’ katika Ofisi za Tume ya Uchaguzi (NEC), Dodoma wakati wa kuchukua fomu za urais. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wakati Tundu Lissu, mgombea urais wa Chama cha Demkrasia na Maendeleo (Chadema), akitangazwa kuchukua fomu ya kugombea urais wiki hii tarehe 8 Agosti 2020, Dk. John Magufuli ndani ya waki hii atachukua fomu.

Mpaka leo, zimebaki siku tano kukamilika wiki ambapo kila mmoja anatarajiwa kufika kwenye ofisi hizo zinazotumia majengo yake mapya yaliyopo katika eneo la Njendengwa, jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo tarehe 5 Agosti 2020, mbele ya waandishi wa jijini Dar es Salaam, Dk. Magufuli ambaye ni Rais wa sasa wa Tanzania, atafika kwenye ofisi za NEC kuchukua fomu ya kugombea urais, hata hivyo hajataja siku, tarehe wala muda wa tukio hilo.

            Soma zaidi:-

 

“Napenda kuwatangazia rasmi kabisa, mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli ambaye sisi kwenye chama chetu ndio muasisi mkubwa wa uwazi, atachukua fomu wiki hii, ni lini nitawaambia tena, lakini wiki hii mgombea CCM atachukua fomu kule jijini Dodoma,” amesema Polepole.

Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020, ambapo NEC imefungua zoezi la uchukuaji fomu ngazi ya urais kuanzia leo na kuhitimishwa tarehe 25 Agosti mwaka huu.

Rais Magufuli alipitishwa na Mkutano Mkuu wa CCM kugombea nafasi hiyo Julai mwaka huu. Rais Magufuli anagombea kwa mara ya pili baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!