Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Naibu Spika Tulia apeta Mbeya, Dk. Kimei chali Vunjo
Habari za Siasa

Naibu Spika Tulia apeta Mbeya, Dk. Kimei chali Vunjo

Dk. Tulia Ackson
Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson ameongoza katika kura za maoni Jimbo la Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM kwa kura 843 kati ya kura zote 885 sawana asilimia 95. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea)

Mshindi wa pili ni Mahenge Mabula aliyepata kura 16 na mshindi wa tatu akiwa ni Charles Mwakipesile aliyepata kura 11.

Iwapo, Dk. Tulia akipitishwa na chama hicho kugombea, ataumana na wagombea wa vyama vingine akiwemo Joseph Mbilinyi maarufu Sugu wa Chadema.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei ameangukia pua Jimbo la Vunjo kwa kupata kura 178 akishika nafasi ya pili na aliyeongoza ni Enock Koola aliyepata kura 187 kati ya 567 zilizopigwa na wajumbe.

Charles Kimei

Nafasi ya tatu imeshikwa na Chrispine Meela aliyepata kura 47, wagombea katika kinyang’anyiro hicho walikuwa 35.

Jimbo la Ismani Mkoa wa Iringa, Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Willium Lukuvi ameongoza kura za maoni kwa kupata kura 453 kati ya 487.

William Lukuvi (wa kwanza kulia)

Wagombea walikuwa tisa ambapo aliyemfuatia amepata kura 16.

Naye mbunge anayemaliza muda wake wa Mufundi Mjini, Cosato Chumi ameongoza kura za maoni kwa kupata kura 135 akifiatiwa na Bazir Tweve kura 122. 

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!