Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Mtulia chali Kinondoni, Tarimba apeta
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Mtulia chali Kinondoni, Tarimba apeta

Maulid Mtulia
Spread the love

MAULID Mtulia, Mbunge anayemaliza muda wake jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, ameshindwa kutetea nafasi yake katika kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Mtulia ameangushwa na Abbas Tarimba katika kura hizo za maoni zilizofanyika leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 katika Ukumbi wa King Solomon.

Wagombea walikuwa 79 ambapo Tarimba amepata kura 171, mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Iddi Azzan kura 77 na Mtulia kura 11 kati ya kura zote 404 zilizopigwa na wajumbe wote.

Wagombea wengine wamekukuta wakipata sifuri, kura moja, tatu au nne.
Matokeo hayo yametangazwa na Frank Kamugisha, msimamizi wa uchaguzi na mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam.

        Soma zaidi:

https://www.youtube.com/watch?v=HrgzMOSHohw

Katika uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba 2015, Mtulia alishinda akiwa Chama Cha Wananchi (CUF) lakini tarehe 2 Desemba 2017 alitangaza kujizulu nafasi hiyo na kuhamia CCM kuunga juhudi zinazofanywa na Serikali chini ya Rais John Magufuli.

Uchaguzi uliporudiwa, CCM ilimpitisha tena Mtulia kuwania nafasi hiyohiyo na kuibuka mshindi tena akimshinda Salum Mwalimu wa Chadema.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!