Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kura za maoni CCM: Msimamizi aonya vurugu ukumbini 
Habari za Siasa

Kura za maoni CCM: Msimamizi aonya vurugu ukumbini 

Msimamizi wa uchaguzi wa kura za maoni jimbo la Mufundi Kusini Mkoa wa Iringa, Sadik Kadulo akizungumza na wajumbe na watia nia.
Spread the love

MSIMAMIZI wa uchaguzi kura za maoni jimbo la Mufindi Kusini wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sadiki Kadulo amewataka wajumbe na watia nia kufuata utaratibu ili kuepusha vurugu ukumbini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea)

Kadulo amesema hayo leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 wakati akitoa utaratibu jinsi ya wajumbe watakavyopiga kura za maoni kuchagua mgombea wanaye mtaka.

Amesema kura za maoni ni sehemu ya mchakato wa uteuzi, lakini kuteuliwa itategemea na sifa na matendo ya mgombea.

Aidha amesema, mgombea ama mjumbe ambaye hatofuata utaratibu hawatasita kumtoa ukumbini.

“Ni imani yangu mkutano utakuwa huru na haki kwani uchaguzi ni sehemu ya demokrasia,” amesema.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya wa Mufindi katika jimbo la Mufindi Kusini

Jimbo la Mufindi Kusini lina wajumbe 612 waliofika katika ukumbi huo ni 604 ambao ndio wajumbe halali wa mkutano huo huku jimbo likiwa na kata 16.

Waliojitokeza kuwania nafasi hiyo ni 31 akiwamo mbunge anayemaliza muda wake, Mendrad Kigola.

Endelea kufuatulia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!