WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kigamboni jijini Dar es Dar es Salaam wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatarajia kupiga kura za maoni za ubunge. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).
Mkutano huo unafanyika leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 katika ukumbi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere, Kivukoni ambapo wagombea ni 78 akiwamo mbunge anayemaliza muda wake, Dk. Faustine Ndugulile.
Wengine ni; aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda pamoja na mchekeshaji maarufu nchini Mpoki Mujuni.
Tayari watia nia 30 kati ya 78 wameshajinadi kwa dakika chache kwa kila mmoja na zoezi hilo bado linaendelea.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi
Leave a comment