Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Yametimia: Membe kuelekea ACT- Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

Yametimia: Membe kuelekea ACT- Wazalendo

Spread the love

SASA ni dhahiri kuwa Bernard Kamilius Membe, waziri wa zamani wa mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa nchini Tanzania, yuko mbioni kujiunga na ACT – Wazalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi wandamizi wa ACT- Wazalendo zinasema, majadiliano kati ya mwanasiasa huyo na viongozi hao juu ya kujiunga kwake na chama hicho, tayari yamekamilika.

“Huyu bwana yuko njiani kujiunga na chama chake,” ameeleza mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho na kuongeza, “kila kitu kimekamilika na muda wowote kutoka sasa, atatangaza adhima hiyo.”

Picha kwenye mitandao ya kijamii zinawaonyesha viongozi wandamizi wa ACT- Wazalendo, wakiongozwa na Maalim Seif Shariff Hamad, wakiwa na majadiliano na mwanasiasa huyo, yenye lengo la kuweka mambo sawa.

MwanaHALISI Online halijaweza kumpata Membe wala viongozi wengine wandamizi wa ACT- Wazalendo, kueleza kwa undani ni lini kiongozi huyo atajiunga na chama chao.

Kupatikana kwa taarifa kuwa Membe yuko mbioni kujiunga na chama hicho cha upinzani nchini, kumekuja siku moja baada ya kilichokuwa chama chake – Chama Cha Mapinduzi – kutangaza kubariki maamuzi ya kumfuta uwanachama.

Membe alikuwa kwenye msuguano na CCM, tangu alipoonesha nia ya kutaka kumpinga rais wa sasa, Dk. John Pombe Magufuli, kupitia chama hicho.

Aidha, katika siku za hivi karibu, Membe amekuwa akitoa kauli zenye kukosoa mchakato wa utafutaji mgombea urais wa Tanzania ndani ya chama hicho tawala, kwa madai kuwa umegubikwa na vitisho.

Katika mahojiano yake na Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani (D.W), Membe alieleza kuwa takribani wanachama sita wa CCM walitaka kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ya juu nchini Tanzania, lakini waliogopa kufanya hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!