Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shamsi Nahodha ataka urais Z’bar
Habari za Siasa

Shamsi Nahodha ataka urais Z’bar

Spread the love

SHAMSI Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, amejitokeza kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Mwanasiasa huyo mkongwe, amechukua fomu hiyo leo asubuhi tarehe 18 Juni 2020, katika Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui.

“Nakishukuru chama changu kwa yote kilichonifanyia kwa muda wote, na kunipa heshma hii kubwa ya kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama chetu cha mapinduzi.

“Nina hakika, watu wengi na wanachama wengi wangetamani sana Mwenyezi Mungu awape fursa hii, wengine watafanikiwa na wengine hawatafanikiwa,” amesema Nahodha muda mfupi baada ya kuchukua fomu.

Nahodha aliyehudumu nafasi ya Waziri Kiongozi katika Serikali ya Zanzibar kwa miaka 10 (2000 – 2010), anakuwa mgombea wa sita akitanguliwa na makada wengine wa chama hicho ambao ni Hussein Ali Mwinyi, Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi, Omar Sheha Mussa na Balozi Ali Karume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!