Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shamsi Nahodha ataka urais Z’bar
Habari za Siasa

Shamsi Nahodha ataka urais Z’bar

Spread the love

SHAMSI Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, amejitokeza kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Mwanasiasa huyo mkongwe, amechukua fomu hiyo leo asubuhi tarehe 18 Juni 2020, katika Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui.

“Nakishukuru chama changu kwa yote kilichonifanyia kwa muda wote, na kunipa heshma hii kubwa ya kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama chetu cha mapinduzi.

“Nina hakika, watu wengi na wanachama wengi wangetamani sana Mwenyezi Mungu awape fursa hii, wengine watafanikiwa na wengine hawatafanikiwa,” amesema Nahodha muda mfupi baada ya kuchukua fomu.

Nahodha aliyehudumu nafasi ya Waziri Kiongozi katika Serikali ya Zanzibar kwa miaka 10 (2000 – 2010), anakuwa mgombea wa sita akitanguliwa na makada wengine wa chama hicho ambao ni Hussein Ali Mwinyi, Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi, Omar Sheha Mussa na Balozi Ali Karume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!