Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai: Rais amesaini miswada sita
Habari za Siasa

Spika Ndugai: Rais amesaini miswada sita

Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesaini miswada sita iliyopitishwa na Bunge la 11. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Miswada hiyo ni Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali namba 2 ya mwaka 2020, Muswada wa Sheria ya Mimea ya mwaka 2020, Muswada wa Sheria ya kusimamia na kuendeleza uvuvi wa bahari kuu 2020.

Muswada wa Sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 3 2020, muswada wa Sheria ya Matumizi ya Fedha za Serikali ya mwaka 2020 na muswada wa mwisho ni Sheria ya Fedha 2020.

Taraifa hiyo imetoelewa leo Jumanne tarehe 16 Juni 2020 na Spika Job Ndugai, katika shughuli ya kufungwa kwa shughuli za Bunge la 11 jijini Dodoma.

“Kwa utendaji kazi wa rais wa namna ambayo isiyokuwa na ulinganifu, tayari ameshatia sahihi misiwada yote hiyo sita, ikiwa pamoja na ile sheria tuliyomaliza jana usiku saa 2 sheria ya fedha namba 8/2020, na yenyewe imetiwa saini tayari, kwenye kumbukumbu zetu miswada yote imepata kibali cha rais na ni sheria za nchi,” amesema Spika Ndugai.

Spika Ndugai amesema, kwa sasa miswada hiyo imekuwa sheria, ikiwemo Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali namba 2, sheria namba 3 ya mwaka 2020 , Sheria ya Afya ya Mimea namba 4 ya mwaka 2020.

Na Sheria ya Kusimamia na kuendeleza  uvuvi wa bahari kuu sheria namba 5 2020, na sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 3 kifungu cha 6 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!