Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Siondoki Chadema, nitagombea tena Ubungo
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Siondoki Chadema, nitagombea tena Ubungo

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema atagombea tena jimbo hilo kupitia chama hicho, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kubenea ametangaza uamuzi huo leo Jumamosi tarehe 13 Juni 2020 jijini Dar es Salaam, katika mkutano wake uliolenga kueleza aliyoyafanya katika kipindi cha miaka mitano kwa  wadau wa jimbo la Ubungo.

Kubenea amesema muda wa uchukuaji fomu katika chama chake ukifika, atajitokeza katika kinyang’anyiro hicho.

Kubenea amesema, anaamini Kamati Kuu ya Chadema itampitisha tena kugombea jimbo hilo huku akisisitiza, hana mpango wa kuondoka katika chama hicho.

“Muda ukifika wa uchukuaji fomu katika Jimbo la Ubungo, nami nakusudia kuchukua na kugombea tena. Naomba mpuuze kauli za mitaani,” amesema Kubenea.

“Mimi niko Chadema, siondoki Chadema, nitagombea ubunge na naamini Kamati Kuu ya Chadema itanipitisha kwa sababu zilezile ilizotumia katika uchaguzi uliopita,” amesema Kubenea huku akishangiliwa na wadau waliojitokeza kumsikiliza.

Kauli hiyo ya msisitizo ya Kubenea kuhusu kutohama Chadema, imekuja kufuata tuhuma kadhaa kutoka kwa baadhi ya watu kwamba anataka kuondoka kwenye chama hicho na kugombea Ubunge kupitia chama kingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!