Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Siondoki Chadema, nitagombea tena Ubungo
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Siondoki Chadema, nitagombea tena Ubungo

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema atagombea tena jimbo hilo kupitia chama hicho, katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kubenea ametangaza uamuzi huo leo Jumamosi tarehe 13 Juni 2020 jijini Dar es Salaam, katika mkutano wake uliolenga kueleza aliyoyafanya katika kipindi cha miaka mitano kwa  wadau wa jimbo la Ubungo.

Kubenea amesema muda wa uchukuaji fomu katika chama chake ukifika, atajitokeza katika kinyang’anyiro hicho.

Kubenea amesema, anaamini Kamati Kuu ya Chadema itampitisha tena kugombea jimbo hilo huku akisisitiza, hana mpango wa kuondoka katika chama hicho.

“Muda ukifika wa uchukuaji fomu katika Jimbo la Ubungo, nami nakusudia kuchukua na kugombea tena. Naomba mpuuze kauli za mitaani,” amesema Kubenea.

“Mimi niko Chadema, siondoki Chadema, nitagombea ubunge na naamini Kamati Kuu ya Chadema itanipitisha kwa sababu zilezile ilizotumia katika uchaguzi uliopita,” amesema Kubenea huku akishangiliwa na wadau waliojitokeza kumsikiliza.

Kauli hiyo ya msisitizo ya Kubenea kuhusu kutohama Chadema, imekuja kufuata tuhuma kadhaa kutoka kwa baadhi ya watu kwamba anataka kuondoka kwenye chama hicho na kugombea Ubunge kupitia chama kingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!