Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe ahamishiwa Hospitali ya Aga Khani Dar
Habari za Siasa

Mbowe ahamishiwa Hospitali ya Aga Khani Dar

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akipandiswa kwenye Ambulance kwa ajili ya kuelekea Airport kwenda Dar Es Salaam kwa Matibabu Zaidi.
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzania Bungeni nchini Tanzania amehamishiwa Hospitali ya Aga Khani, Dar es Salaam kwa matibabu zaidi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mbowe alikuwa amelazwa Hospitali binafsi jijini Dodoma baada ya kudaiwa kushambuliwa na watu wasiojulikana katika makazi yake Area D jijini humo usiku wa kuamkia leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020.

Mapema leo asubuhi, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliueleza umma wa Watanzania kwamba wanafanya mpango wa kumhamishiwa Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.

Leo jioni, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene ametoa taarifa akisema,”Mwenyekiti wa Chama Taifa na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni (KUB), Mhe. Freeman Mbowe (Mb), amepokelewa muda mfupi uliopita Kitengo cha dharura Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya uchunguzi wa matibabu zaidi.”

Endelea kufuatilia MwanaHalisi Online & TV kwa habari zaidi

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!