Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yapuliza kipyenga cha Urais
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yapuliza kipyenga cha Urais

John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia ya Maendeleo (Chadema) kimefungua milango kwa watia nia wa urais wa chama hicho kuanzia leo Jumatano tarehe 3, Juni hadi Juni 15,2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu wa Chadema, Katibu Mkuu chama hicho, John Mnyika amesema watia nia hao wataandika barua kwa katibu mkuu.

Amesema, baada ya hapo, atafikisha majina ya waliojitokeza kwa kamati kuu ambayo itayapitia,”tutatoa taarifa tena ya nini kitaendelea baada ya tarehe 15 Juni 2020.”

Pia, Mnyika amesema, chama hiko kimefungua milango ya majadiliano na vyama vingine vya siasa,”vyenye dhamira ya kuiondoa CCM madarakani, tutashirikiana nao.”

Kuhusu waliotia nia mapema kama alivyofanya Dk Myrose Majige ya kutangaza, amesema,”ili utie nia, lazima uandike barua kwa katibu mkuu, lakini kama umetia nia huko kwenye vyombo vya habari, mimi siwezi kuwazungumzia.

Mnyika amewataka watia nia wote kuhakikisha wanasoma vyema mwongozo wa chama hicho wa mwaka 2012 unaodhibiti rushwa ndani ya chama.

“Wagombea wanaotarajia kutia nia, wazingatie mwongozo na kama hawatofuata, chama hakitasita kuwachukulia hatua,” amesema Mnyika

Kuhusu ubunge, uwakilishi na udiwani, Mnyika amesema, utaratibu utatangazwa baadaye.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!