Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Biashara holela zamuibia mbunge, waziri amjibu
Habari Mchanganyiko

Biashara holela zamuibia mbunge, waziri amjibu

Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Asha Abdallah Juma
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Asha Abdallah Juma ameitaka Serikali ya Tanzania kueleza jinsi ilivyojipanga katika udhibiti wa ufanyaje wa biashara holela unaofanywa na wafanyabiashara ndogondogo ambao walipewa vitambulisho vya machinga. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Katika swali la Asha aliloliuliza leo Jumanne tarehe 26 Mei, 2020 bungeni kwa njia ya kidigitali na kujibiwa kwa mfumo huo huo, amesema, zoezi la kuwapatia vitambulisho wajasiriamali wamachinga limefanyika vizuri na kuendelea kufanya biashara zao mahali popote.

“Je, Serikali imejipanga vipi ili kuhakikisha kuwa na usimamizi na udhibiti katika ufanyaji wa biashara holela,” amehoji Asha

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi amesem, Serikali kupitia wizara ya fedha na mipango kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – Tamisemi imetunga Kanuni za Usimamizi wa Kodi (Usajili wa Wafanyabiashara Wadogo na Watoa Huduma) za mwaka 2020.

Amesema, kwa mujibu wa kanuni hizo, mamlaka za serikali za mitaa zimeelekezwa kusimamia na kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara na watoa huduma wadogo ili kuhakikisha biashara holela zinadhibitiwa.

“Udhibiti na usimamizi utafanyika wakati wa kusajili na kuwapatia vitambulisho wajasiriamali wadogo kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi na kuhakikisha wanaendesha shughuli zao pasipo kubugudhiwa.”

“Sambamba na kanuni hizo, Serikali imeandaa mwongozo wa usimamizi wa wafanyabiashara wadogo na watoa huduma wadogo ambao umeainisha majukumu ya kila mdau katika usimamizi wa wafanyabiashara wadogo na watoa huduma wadogo,” amesema waziri huyo katika majibu yake

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!