Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Biashara holela zamuibia mbunge, waziri amjibu
Habari Mchanganyiko

Biashara holela zamuibia mbunge, waziri amjibu

Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Asha Abdallah Juma
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Asha Abdallah Juma ameitaka Serikali ya Tanzania kueleza jinsi ilivyojipanga katika udhibiti wa ufanyaje wa biashara holela unaofanywa na wafanyabiashara ndogondogo ambao walipewa vitambulisho vya machinga. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Katika swali la Asha aliloliuliza leo Jumanne tarehe 26 Mei, 2020 bungeni kwa njia ya kidigitali na kujibiwa kwa mfumo huo huo, amesema, zoezi la kuwapatia vitambulisho wajasiriamali wamachinga limefanyika vizuri na kuendelea kufanya biashara zao mahali popote.

“Je, Serikali imejipanga vipi ili kuhakikisha kuwa na usimamizi na udhibiti katika ufanyaji wa biashara holela,” amehoji Asha

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi amesem, Serikali kupitia wizara ya fedha na mipango kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – Tamisemi imetunga Kanuni za Usimamizi wa Kodi (Usajili wa Wafanyabiashara Wadogo na Watoa Huduma) za mwaka 2020.

Amesema, kwa mujibu wa kanuni hizo, mamlaka za serikali za mitaa zimeelekezwa kusimamia na kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara na watoa huduma wadogo ili kuhakikisha biashara holela zinadhibitiwa.

“Udhibiti na usimamizi utafanyika wakati wa kusajili na kuwapatia vitambulisho wajasiriamali wadogo kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi na kuhakikisha wanaendesha shughuli zao pasipo kubugudhiwa.”

“Sambamba na kanuni hizo, Serikali imeandaa mwongozo wa usimamizi wa wafanyabiashara wadogo na watoa huduma wadogo ambao umeainisha majukumu ya kila mdau katika usimamizi wa wafanyabiashara wadogo na watoa huduma wadogo,” amesema waziri huyo katika majibu yake

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!