Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makonda atoa siku 10 Hospitali ya Kigamboni ianze kazi
Habari Mchanganyiko

Makonda atoa siku 10 Hospitali ya Kigamboni ianze kazi

Paul Makonda, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ametoa siku kumi kwa uongozi wa Manispaa ya Kigamboni kuhakikisha Hospital wilaya hiyo inaanza kutoa huduma kwa wananchi ifikapo tarehe 1 June, 2020 baada ya Majengo yote ya Hospital hiyo kukamilika. Anandika Hamis Mguta, Dar es salaam…(endelea).

RC Makonda ametoa agizo hilo leo Ijumaa tarehe 22 Mei, 2020 wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo wilayani humo.

Katika ziara hiyo, Makonda amekabidhi Magodoro 175, Mashuka 1,294 na Ndoo na kueleza ifikapo Jumanne ya wiki ijayo atakabidhi tena Mashine mbili za Ultrasound zenye thamani ya Sh. 70 milioni na Vitanda 100 ili kuhakikisha huduma zinaanza kutolewa.

Aidha RC Makonda amemuelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa huo kuhakikisha anapeleka watumishi 40 kwenye hospital hiyo kwaajili ya kutoa huduma ili kutimiza lengo la Serikali ya Awamu ya Tano la kupunguza kero za Afya kwa Wananchi.

Hospitali mpya ya wilaya ya Kigamboni

Akiwa katika ukaguzi wa Ujenzi wa Barabara na Round about inayounganisha barabara za kuelekea Feri na Kibada kutokea Daraja la Mwalimu Nyerere, Makonda amewaelekeza Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD) kuhakikisha ujenzi wa barabara na mzunguko wa magari vinakamilika na kukabidhiwa kabla ya Septemba 2020.

Pamoja na hayo, Makonda amewaelekeza Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Watendaji wa Jiji hilo kuhakikisha maelekezo na ahadi zote zinazotolewa na Rais John Magufuli vinatekelezwa kwa wakati pasipo kushurutishwa huku akiwataka Wakandarasi wote kuhakikisha miradi yao inakamilika kwa wakati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!