Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bunge lataka Serikali iisaidie Tanesco ilipwe mabilioni
Habari Mchanganyiko

Bunge lataka Serikali iisaidie Tanesco ilipwe mabilioni

Makao Mkuu wa Tanesco, Ubungo Dar es Salaam kabla hayajavunjwa
Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge  ya Hesabu za Serikali (PAC) nchini Tanzania, imeishauri Serikali kuhakikisha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), linalipwa fedha  zaidi ya  Sh. 454  bilioni, inazodai kutoka taasisi za umma na wateja binafsi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Ijumaa tarehe 22 Mei 2020, bungeni jijini Dodoma na, Makamu Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilaly wakati anawasilisha taarifa ya kamati hiyo, kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni, 2019.

Hilaly amesema, kwa mujibu wa taarifa ya CAG, hadi kufikia tarehe 30 Juni 2019, TANESCO inadai taasisi za Serikali Sh. 205.8 bilioni, wateja binafsi Sh. 199.3 na madeni mengine Sh. 49 bilioni.

Amesema, deni hilo linasababisha hali ya ukwasi ya shirika hilo kupungua na kuathiri utendaji wake, ikiwemo kugharamia shughuli mbalimbali.  

Hilaly  ambaye ni mbunge wa Sumbawanga Mjini kupitia CCM amesema, PAC imeishauri Serikali ichukue jitihada mahsusi za kibajeti kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, kuhakikisha taasisi zote za serikali zinazodaiwa na TANESCO zinalipa madeni yao.   

“Serikali ichukue jitihada mahsusi za kibajeti kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha taasisi zote za Serikali zinazodaiwa na TANESCO zinalipa madeni yao kwa kuzingatia utaratibu wa kibajeti utakaowekwa na Hazina,”amesema Hilaly

Aidha, Hilaly amesema, Bunge limeshauri uongozi wa TANESCO, uimarishe mikakati ya ukusanyaji madeni ili fedha hizo zipatikane kwa wakati.  

“Uwepo wa deni hilo, unaathiri hali ya utendaji wa kila siku wa TANESCO na unaharibu taswira halisi ya taarifa za hesabu za shirika, kwa hiyo basi, Bunge linaazimia kwamba, Menejimenti ya TANESCO iimarishe mikakati ya ukusanyaji wa madeni ili kuhakikisha madeni husika yanakusanywa kwa wakati,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!