Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Madereva 23 wa Tanzania wakutwa na corona, wazuiwa kuingia Kenya
Habari Mchanganyiko

Madereva 23 wa Tanzania wakutwa na corona, wazuiwa kuingia Kenya

Spread the love

SERIKALI ya Kenya imewazuia madareva 25 wakiwamo 23 wa Tanzania kuingia nchini humo baada ya kuwapima na kuwakuta na maambukizo ya virufi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Madereva wengine wawili, mmoja anatoka Uganda na mwingine wa Rwanda.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano tarehe 13 Mei 2020, naibu waziri wa Afya, Dk Rashid Aman amesema madereva hao walipimwa katika kipindi cha saa 24 na kukutwa na maambukizo ya COVID-19.

Wizara hiyo imesema kwamba hatua hiyo inalenga kuwalinda Wakenya dhidi ya maambukizi kutoka kwa raia wa kigeni.

Amesema katika mapambano ya COVID-19, wanatarajia kuanzisha maabara mbili za kuhama ili kuongeza upimaji zitakazowekwa mpaka wa Namanga.

Dk Aman amewataka Wakenya kuchukua tahadhari na kuwaripoti watu ambao wanawashuku kuingia nchini humo kwa njia za panya.

Katika maelezo yake, Dk Aman amesema wagonjwa wapya 22 wameripotiwa nchini humo hivyo kwa sasa Taifa hilo idadi ya wagonjwa wa Covid-19 wamefikia 737.

Dk Aman amesema idadi hiyo inatokana na watu 1,516 waliopimwa katika muda wa saa 24 zilizopita.

Amesema mpaka sasa, Kenya imefanikiwa kuwapima watu 35, 432.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!