Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ataka gongo itumike kuikabili corona
Habari za Siasa

Mbunge ataka gongo itumike kuikabili corona

Spread the love

PROFESA  Jumanne Kishimba, Mbunge wa Kahama (CCM), ameishauri serikali kuruhusu pombe ya gongo, itumike katika kukabiliana na mlipuko wa Virusi vya Corona, kwa wananchi wasio na uwezo wa kununua vitakasa mikono (Sanitizer). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Prof. Kishimba ametoa ushauri huo jana tarehe 6 Aprili 2020, bungeni jijini Dodoma.

Amemuomba Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, kuruhusu matumizi ya pombe hiyo kwa kuwa ina kiwango cha kilevi kinachokaribiana na kiwango cha vitakasa mikono.

“Tunamuomba waziri wa afya sasa, kwa kiwa wananchi hawawezi kununua sabuni tunazotumia ambazo zina alcohol asilimia 65, atamke kwa muda huu wa dharura wananchi wanawie gongo ili kuzuia suala la Corona,” amesema Prof. Kishimba na kuongeza:

“Mheshimiwa Spika sanitizer ina alcohol asilimia 65 na gongo ina asilimia 55, inaonekana inafaa kuliko spiriti zilizopo.”  Kwa mujibu wa serikali, Tanzania ina idadi ya wagonjwa 24 wa COVID-19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!