Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ataka gongo itumike kuikabili corona
Habari za Siasa

Mbunge ataka gongo itumike kuikabili corona

Spread the love

PROFESA  Jumanne Kishimba, Mbunge wa Kahama (CCM), ameishauri serikali kuruhusu pombe ya gongo, itumike katika kukabiliana na mlipuko wa Virusi vya Corona, kwa wananchi wasio na uwezo wa kununua vitakasa mikono (Sanitizer). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Prof. Kishimba ametoa ushauri huo jana tarehe 6 Aprili 2020, bungeni jijini Dodoma.

Amemuomba Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, kuruhusu matumizi ya pombe hiyo kwa kuwa ina kiwango cha kilevi kinachokaribiana na kiwango cha vitakasa mikono.

“Tunamuomba waziri wa afya sasa, kwa kiwa wananchi hawawezi kununua sabuni tunazotumia ambazo zina alcohol asilimia 65, atamke kwa muda huu wa dharura wananchi wanawie gongo ili kuzuia suala la Corona,” amesema Prof. Kishimba na kuongeza:

“Mheshimiwa Spika sanitizer ina alcohol asilimia 65 na gongo ina asilimia 55, inaonekana inafaa kuliko spiriti zilizopo.”  Kwa mujibu wa serikali, Tanzania ina idadi ya wagonjwa 24 wa COVID-19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!