Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif awaangukia Watanzania
Habari za Siasa

Maalim Seif awaangukia Watanzania

Spread the love

MAALIM Seif Shariff Hamad, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, amewasihi Watanzania kuchukua tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19). Anaripoti Jabir Idrisa, Zanzibar … (endelea).

Maalim Seif ametoa wito huo leo tarehe 27 Machi 2020, wakati akihojiwa na Kituo cha Redio cha Bomba FM, Visiwani Zanzibar.

Maalim Seif amewaomba wananchi wote kufuata maelekezo yanayotolewa na watalaamu wa afya, kwa ajili ya kudhibiti ueneaji wa ugonjwa huo.

“Wananchi wote wa Tanzania tudumishe usafi, hakikisha kila mara tukoshe mikono yetu kwa kutumia maji tiririka na sabuni, tuepuka sana mikusanyiko, natoa Wito kwa Madereva wa dala dala kuhakikisha wanapinguza ujazaji wa abiria ili kutowa nafasi yakuepusha mbanano,” ameshauri Maalim Seif.

Wakati huo huo, Maalim Seif ameiomba Serikali ishirikiane na Vyama vya Siasa katika mapambano ya kudhibiti ugonjwa huo.

Serikali ishirikishe vyama vya siasa katika vita hivi vya janga la Corona umoja wa kitaifa ni muhimu sana, tuache kuingiza tofauti za kisiasa, wito wangu tuwe wamoja. Tuko tayari kushirikiana na serikali zote mbili kupambana na janga hili la Corona,” amesema Maalim Seif.

Hadi sasa serikali imetangaza kwamba, kuna wagonjwa 13 wa COVID-19, ambao wanaendelea vizuri.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!