Friday , 3 May 2024
Habari za Siasa

Lema asakwa Dar

Godbless Lema, Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema)
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linadaiwa kuzingira Hoteli ya Regency Park iliyoko Mikocheni, jijini Dar es Salaam likimsaka Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Lema kupitia ukurasa wake wa twitter leo tarehe 17 Machi 2020, ameandika kwamba, polisi kadhaa waliovaa kiraia wamezingira hoteli hiyo.

“Polisi wengi wakiwa na magari wamevamia Hotel ninayo fikia Regency Park Mikocheni, nimepata taarifa kuwa wananitafuta,” ameandika Lema.

Chadema katika ukurasa wake wa twitter kimeeleza kwamba, hadi sasa hakijafahamu sababu za mbunge wake kusakwa na polisi.

https://twitter.com/godbless_lema/status/1239793753604395009

Na kwamba, Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, alipanga kufanya mkutano na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, kujibu kauli ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, DPP Biswalo Mganga, kwamba atamfungulia kesi kutokana na kutoa taarifa za uongoz juu ya Jeshi la Polisi mkoani Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!