Saturday , 27 April 2024
Habari za Siasa

Lema asakwa Dar

Godbless Lema, Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema)
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linadaiwa kuzingira Hoteli ya Regency Park iliyoko Mikocheni, jijini Dar es Salaam likimsaka Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Lema kupitia ukurasa wake wa twitter leo tarehe 17 Machi 2020, ameandika kwamba, polisi kadhaa waliovaa kiraia wamezingira hoteli hiyo.

“Polisi wengi wakiwa na magari wamevamia Hotel ninayo fikia Regency Park Mikocheni, nimepata taarifa kuwa wananitafuta,” ameandika Lema.

Chadema katika ukurasa wake wa twitter kimeeleza kwamba, hadi sasa hakijafahamu sababu za mbunge wake kusakwa na polisi.

https://twitter.com/godbless_lema/status/1239793753604395009

Na kwamba, Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, alipanga kufanya mkutano na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, kujibu kauli ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, DPP Biswalo Mganga, kwamba atamfungulia kesi kutokana na kutoa taarifa za uongoz juu ya Jeshi la Polisi mkoani Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!