Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sensa kubaini wasio na ajira yaja
Habari za Siasa

Sensa kubaini wasio na ajira yaja

Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira.
Spread the love

ANTONY Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Ajira na Vijana amesema serikali itaifanyia kazi hoja ya Grace Tendega, Mbunge Viti Maalumu (Chadema), ya kufanya sensa ili kubaini idadi ya vijana wasiokuwa na ajira. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Mavunde ametoa ahadi hiyo jana tarehe 6 Februari 2020 bungeni jijini Dodoma, baada ya Tendega kuitaka serikali kubaini vijana wazurulaji na wanaocheza mchezo wa ‘Pool Table’ wakati wa kazi, kutokana na kukosa ajira.

Naibu Waziri huyo anayeshughulikia masuala ya vijana na ajira, amesema suala hilo litawasilishwa katika Ofisi ya Taifa ya Takwimu, ili ifanyiwe kazi katika sensa ya watu na makazi, itakayofanyika mwaka 2022.

Akizungumzia kuhusu changamoto ya ajira, Mavunde amesema serikali inaendelea kuitatua kupitia njia mbalimbali, ikiwemo kutenga maeneo maalumu ya uzalishaji mali kwa vijana zaidi ya ekari 217,882.36, ambazo zina kidhi shughuli za kilimo, viwanda na biashara ndogo.

Kuboresha mazingira ya uwekezaji hasa katika sekta zinazozalisha nafasi nyingi za ajira,  ikiwemo sekta ya kilimo, ufugaji, uvuvi, madini na viwanda.

Pia, Mavunde amesema serikali imeanzisha vituo vya maendeleo ya vijana,  majengo ya viwanda pamoja na kuwajengea ujuzi, kupitia programu ya kukuza ujuzi nchini, ili kwa kutumia mafunzo mbalimbali vijana waweze kujiajiri.

“Kwa mwaka huu wa fedha, Serikali inatekeleza mafunzo ya stadi mbalimbali za kazi ambapo jumla ya vijana 49,265 watanufaika, kuweka mazingira bora ya uwekezaji nchini ili kuvutia uwekezaji mkubwa kwenye sekta zenye uwezo mkubwa wa kuzalisha ajira hususani kilimo, ufugaji, madini na Viwanda,” amesema Mavunde.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!