Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zungu aukwaa uwaziri, Simbachawene amrithi Lugola
Habari za Siasa

Zungu aukwaa uwaziri, Simbachawene amrithi Lugola

Spread the love

RAIS John Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, kwa kumteua Mussa Zungu, Mbunge wa Ilala kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, akichukua nafasi ya George Simbachawene. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mabadiliko hayo yametangazwa leo tarehe 23 Januari 2020, na Katibu Mkuu  Kiongozi Ikulu, Balozi John Kijazi.

Kwa mujibu wa Balozi Kijazi, Simbachawene aliyemhamishia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, amechukua nafasi ya Kangi Lugola, ambaye uteuzi wake umetenguliwa leo na Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameteua mabalozi watatu, akiwemo Jenerali Jacob Kingu, aliyejiuzulu Ukatibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuwa Balozi.

Balozi Kijazi amesema  vituo vya kazi vya mabalozi hao, vitatangazwa baadae.

Pia, Balozi Kijazi amesema Rais Magufuli amewaongezea muda wa miaka 2, mabalozi saba, akiwemo Asha Rose Migiro, Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, George Madafa Balozi wa Tanzania nchini Italia na Emmanuel Nchimbi (Brazil).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!