Saturday , 27 April 2024
Habari za Siasa

Mbowe awindwa Hai

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anawindwa jimboni kwake Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), amemwelekeza Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai kufuata fedha za mfuko wa Jimbo la Hai na kupanga matumizi.

Amesema, fedha hizo Sh. 42 milioni zipo kwa Mbowe tangu mwaka 2018/19 na hazijapangiwa matumizi, na sasa miaka miwili imepita bila kutumika.

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, tarehe 8 Januari 2020, Waitara amesema, mwenye mamlaka ya kupanga matumizi ya fedha hizo si Mbowe bali ni Mkuu wa Wilaya na mkurugenzi.

Mwita amemtaka Sabaya kumwagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo kufanya utaratibu wa kupata fedha na kupanga matumizi yake naye (Sabaya) kusimamia.

Pia amemtuhumu Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, kwamba amekuwa mtoro na hafanyi kazi za jimbo, na amekuwa akifanya matumizi ya fedha hizo kwa njia ya simu, kitu ambacho hakikubaliki.

MwanaHALISI Online leo tarehe 9 Januari 2020, limemtafuta Mbowe ili kupata ufafanuzi kuhusu tuhuma hizo bila mafanikio. Na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi wa maneno, hajajibu.

Kwenye mkutano huo, Sabaya amemuahidi Mwita kwamba, hakuna fedha zitazochezewa na kwamba, yoyote atakayejaribu kufanya hivyo, atamfyatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!