Sunday , 10 December 2023
Habari za Siasa

Mbowe awindwa Hai

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anawindwa jimboni kwake Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), amemwelekeza Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai kufuata fedha za mfuko wa Jimbo la Hai na kupanga matumizi.

Amesema, fedha hizo Sh. 42 milioni zipo kwa Mbowe tangu mwaka 2018/19 na hazijapangiwa matumizi, na sasa miaka miwili imepita bila kutumika.

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, tarehe 8 Januari 2020, Waitara amesema, mwenye mamlaka ya kupanga matumizi ya fedha hizo si Mbowe bali ni Mkuu wa Wilaya na mkurugenzi.

Mwita amemtaka Sabaya kumwagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo kufanya utaratibu wa kupata fedha na kupanga matumizi yake naye (Sabaya) kusimamia.

Pia amemtuhumu Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, kwamba amekuwa mtoro na hafanyi kazi za jimbo, na amekuwa akifanya matumizi ya fedha hizo kwa njia ya simu, kitu ambacho hakikubaliki.

MwanaHALISI Online leo tarehe 9 Januari 2020, limemtafuta Mbowe ili kupata ufafanuzi kuhusu tuhuma hizo bila mafanikio. Na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi wa maneno, hajajibu.

Kwenye mkutano huo, Sabaya amemuahidi Mwita kwamba, hakuna fedha zitazochezewa na kwamba, yoyote atakayejaribu kufanya hivyo, atamfyatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataka jamii inayohoji mafisadi

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan ametoa maagizo juu ya uboreshaji dira...

Habari za SiasaTangulizi

Kapinga: Kukatika kwa umeme siyo hujuma

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali ipo kazini...

error: Content is protected !!