Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtuhumiwa azidunda kortini kupinga masharti ya dhamana
Habari Mchanganyiko

Mtuhumiwa azidunda kortini kupinga masharti ya dhamana

Daniel Njonjo, Mtuhumiwa wa shtaka la kufanya vurugu Kenya
Spread the love

DANIEL Njonjo, anayetuhumiwa kwa shtaka la kufanya vurugu, amepigana na polisi katika korti ya Mahakama ya Milimani jijini Nairobi, Kenya, akipinga sharti la dhamana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kisa hicho kimetokea jana tarehe 8 Januari 2020, baada ya Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Muthoni Nzibe, kumuamuru mtuhumiwa huyo kutoa Shilingi ya Kenya 30,000, kama sharti la dhamana.

Baada ya mahakama kutoa sharti hilo, Njonjo alianza vurugu na kupelekea kupigana na maafisa polisi wa mahakama hiyo, waliojaribu kumkamata kwa ajili ya kumpeleka rumande.

Katika utetezi wake, Njonjo alisema ni bora afe kuliko kutekeleza sharti hilo, kwa kuwa hana uwezo wa kutoa kiasi hicho cha fedha.

Na kuiomba mahakama hiyo kumuacha kwa dhamana, kwa kuwa hakumuuwa mtu.

Njonjo anatuhumiwa kukutwa na kisu katika Mtaa wa Kimathi jijini Nairobi, Kenya. Na anatarajiwa kurudi tena mahakamani hapo tarehe 22 Januari mwaka huu, siku ambayo kesi yake itakwenda kutajwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!