Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kizimbani kwa kukeketa watoto wake
Habari Mchanganyiko

Kizimbani kwa kukeketa watoto wake

Spread the love

COSMAS Chacha (45), Mkazi wa Kivule, jijini Dar es Salaam amefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa makosa ya ukeketeji watoto wake watatu. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Akisoma mashtaka hayo leo tarehe 6 Januari 2020 Wakili Serikali, Faraji Nguka mbele ya  Hakimu Rashid Chaungu, amedai kuwa tarehe 8 Desemba  2019, katika eneo la kivule jijini Dar es Salaam, mshtkiwa ambaye ni baba mzazi wa watoto hao walio chini ya umri wa miaka 18 na mwenye jukumu la kuwalea, aliwapeleka kukeketwa na kuwasababishia maumivu makali.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mtuhumiwa alikana kutenda makosa hayo na upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Chaungu alitoa masharti ya dhamana ya Sh. 5 milioni kwa wadhamini wawili, lakini mshtakiwa hajatimiza masharti ya dhamana kwa mmoja kukosa utambulisho na barua kutopitia kwa mkurugenzi hivyo amerejeshwa rumande.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 20 Januari 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!