Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kizimbani kwa kukeketa watoto wake
Habari Mchanganyiko

Kizimbani kwa kukeketa watoto wake

Spread the love

COSMAS Chacha (45), Mkazi wa Kivule, jijini Dar es Salaam amefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa makosa ya ukeketeji watoto wake watatu. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Akisoma mashtaka hayo leo tarehe 6 Januari 2020 Wakili Serikali, Faraji Nguka mbele ya  Hakimu Rashid Chaungu, amedai kuwa tarehe 8 Desemba  2019, katika eneo la kivule jijini Dar es Salaam, mshtkiwa ambaye ni baba mzazi wa watoto hao walio chini ya umri wa miaka 18 na mwenye jukumu la kuwalea, aliwapeleka kukeketwa na kuwasababishia maumivu makali.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mtuhumiwa alikana kutenda makosa hayo na upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Chaungu alitoa masharti ya dhamana ya Sh. 5 milioni kwa wadhamini wawili, lakini mshtakiwa hajatimiza masharti ya dhamana kwa mmoja kukosa utambulisho na barua kutopitia kwa mkurugenzi hivyo amerejeshwa rumande.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 20 Januari 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!