Thursday , 7 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Kizimbani kwa kukeketa watoto wake
Habari Mchanganyiko

Kizimbani kwa kukeketa watoto wake

Spread the love

COSMAS Chacha (45), Mkazi wa Kivule, jijini Dar es Salaam amefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa makosa ya ukeketeji watoto wake watatu. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Akisoma mashtaka hayo leo tarehe 6 Januari 2020 Wakili Serikali, Faraji Nguka mbele ya  Hakimu Rashid Chaungu, amedai kuwa tarehe 8 Desemba  2019, katika eneo la kivule jijini Dar es Salaam, mshtkiwa ambaye ni baba mzazi wa watoto hao walio chini ya umri wa miaka 18 na mwenye jukumu la kuwalea, aliwapeleka kukeketwa na kuwasababishia maumivu makali.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mtuhumiwa alikana kutenda makosa hayo na upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Chaungu alitoa masharti ya dhamana ya Sh. 5 milioni kwa wadhamini wawili, lakini mshtakiwa hajatimiza masharti ya dhamana kwa mmoja kukosa utambulisho na barua kutopitia kwa mkurugenzi hivyo amerejeshwa rumande.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 20 Januari 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

error: Content is protected !!