Saturday , 2 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Wanne kizimbani kwa kuiibia polisi Sh 798 milioni
Habari Mchanganyiko

Wanne kizimbani kwa kuiibia polisi Sh 798 milioni

Spread the love

WATU Wanne akiwamo Ofisa wa Jeshi la Polisi, wamepandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kwa makosa ya kuiingizia hasara jeshi hilo na utakatishaji wa fedha kiasi cha Sh 798 milioni. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Leo tarehe 6 Januari 2020 , Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Salum Ali, amesomea mashtaka matatu watuhumiwa hao ambao  ni Emmanuel Mkilia (44), Ofisa wa Polisi; Dolnald Mhaiki (39) mfanyabiashara; Abdi Ally (48), mfanyabiashara na Mohyadini Hussein (56) mfanyabiashara.

Wankyo amewasomea shtaka la kwanza la kuliingizia hasara Jeshi la Polisi kiasi cha Sh 798,789,272.

Shtaka la Pili ni kujiingizia pesa kwa njia ya udanganyifu ambao inadaiwa kutendwa na washtakiwa wote kati ya tarehe 19 Machi 2013 na tarehe 18 Oktoba 2013, ambapo watuhumiwa walidanganya kuwa wamefunga mfumo wa  kitaalamu wa taarifa za washukiwa kwenye vituo vine vya polisi jambo ambalo sio kweli.

Shtaka la mwisho ni utakatishaji fedha haramu ambapo watuhumiwa wote wanadaiwa kutakatisha kiasi cha Shilingi  798,789,272.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari Mchanganyiko

Waziri Bashungwa aagiza wahandisi kujengewa uwezo

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameiagiza Bodi ya Usajili wa...

Habari Mchanganyiko

Heche ataka mawakili vijana kuamka sakata Mpoki

Spread the loveMWENYEKITI wa Mawakili Vijana Tanzania kutoka Chama cha Mawakili wa...

error: Content is protected !!