Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanne kizimbani kwa kuiibia polisi Sh 798 milioni
Habari Mchanganyiko

Wanne kizimbani kwa kuiibia polisi Sh 798 milioni

Spread the love

WATU Wanne akiwamo Ofisa wa Jeshi la Polisi, wamepandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kwa makosa ya kuiingizia hasara jeshi hilo na utakatishaji wa fedha kiasi cha Sh 798 milioni. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Leo tarehe 6 Januari 2020 , Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Salum Ali, amesomea mashtaka matatu watuhumiwa hao ambao  ni Emmanuel Mkilia (44), Ofisa wa Polisi; Dolnald Mhaiki (39) mfanyabiashara; Abdi Ally (48), mfanyabiashara na Mohyadini Hussein (56) mfanyabiashara.

Wankyo amewasomea shtaka la kwanza la kuliingizia hasara Jeshi la Polisi kiasi cha Sh 798,789,272.

Shtaka la Pili ni kujiingizia pesa kwa njia ya udanganyifu ambao inadaiwa kutendwa na washtakiwa wote kati ya tarehe 19 Machi 2013 na tarehe 18 Oktoba 2013, ambapo watuhumiwa walidanganya kuwa wamefunga mfumo wa  kitaalamu wa taarifa za washukiwa kwenye vituo vine vya polisi jambo ambalo sio kweli.

Shtaka la mwisho ni utakatishaji fedha haramu ambapo watuhumiwa wote wanadaiwa kutakatisha kiasi cha Shilingi  798,789,272.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!