Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga, Simba wamlilia Mzee Akilimali
Michezo

Yanga, Simba wamlilia Mzee Akilimali

Marehemu Mzee Ibrahim Akilimali
Spread the love

KLABU ya Yanga imemlilia aliyekuwa Katibu wa Baraza la Wazee wa klabu ya Yanga, Mzee Ibrahim Akilimali, aliyefariki dunia alfajiri ya leo tarehe 14 Desemba 2019, Bagamoyo mkoani Pwani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo iliyotolea asubuhi ya leo, Mzee Akilimali atazikwa kesho tarehe 15 Desemba, 2019 majira ya saa 10 jioni, maeneo ya Tandale kwa Mtogole.

“Klabu ya Yanga inasikitika kutangaza kifo cha Mwanachama wetu Maarufu na Mzee wetu, Ibrahim Akilimali kilichotokea alfajiri ya leo Bagamoyo Mkoani Pwani. Maziko yanatarajiwa kufanyika kesho saa 10 jioni Tandale kwa Mtogole. Innah lillah wainnah ilayh rajiuun. Haikuwa Dunia ila ni mapito,” inaeleza taarifa ya Klabu yaYanga

Haji Manara, Afisa Habari wa Klabu ya Simba ametoa pole kwa familia ya Mzee Akilimali kwa msiba huo mzito.

Pia, Manara amesema Simba itashiriki kikamilifu kwenye msiba huo.

“Tumeondokewa, Mwamba katika Miamba ya kabumbu Nchini umeanguka, Mzee wetu, Baba na Babu yetu, Katibu wa Baraza la Wazee, Yanga Ibrahim Akilimali katangulia mbele ya haki, poleni Familia, poleni Wanayanga,huu ni msiba wetu sote na tutashiriki kikamilifu kwenye majonzi haya,” amesema Manara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

error: Content is protected !!