Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Waziri atia msisitizo uandishi wa Insha
Elimu

Waziri atia msisitizo uandishi wa Insha

Spread the love

WILLIAM Ole Nasha, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, amewataka wakuu wa shule nchini kushawishi wanafunzi kuchangamkia fursa za mashindano ya uandishi wa Insha za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo 11 Desemba 2019, jijini Dodoma hafla ya kutunuku vyeti kwa washindi wa kitaifa wa Shindano la Uandishi wa Insha za SADEC na EAC.

Amesema, uandishi wa Insha za SADEC na EAC utaweza kuwasaidia na kuwaongozea uwezo wanafunzi katika kukuza ujuzi wa lugha.

“Napenda kusisitiza kuwa, wakuu wote wa shule kuendelea kuwashawishi wanafunzi kuchangamkia fursa za mashindano kwani pamoja na kuwaongozea uwezo wao katika kukuza ujuzi wa lugha, uandishi wa insha unaongeza maarifa kwa ujumla,” amesema.

Naibu Waziri huyo aliwataka pia Wakuu hao kusimamia kwa umakini mchakato wa mashindano hayo ili kuhakikisha ushiriki wa wanafunzi wengi.

“Nawaagiza kila Mkuu wa shule kuteua mratibu atakayefanya kazi ya kusimamia wanafunzi ili wazingatie na kufuata taratibu zote za uandishi wa insha ili tuweze insha nzuri na kuziwasilisha katika mashindano ya kanda,”amesema.

Naye,Mratibu wa Shindano hilo,Sylvia Chinguwile alimtangaza, Vanessa Lema kutoka Shule ya Sekondari Longodo Mkoani Arusha  ambaye yupo kidato cha nne kuwa mshindi wa shindano hilo.

Wengine walioshinda katika shindano hilo ni Thomas Kalisha mwanafunzi wa kidato cha tatu kutoka shule ya Kibasila  ya Jijini Dar es salaam ambaye alishika nafasi ya pili,huku nafasi ya tatu ikishikwa na Monica Nyamhanga mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Heritage ya Mkoani Pwani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!