Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe kuongoza kikao cha ‘machinjio’
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe kuongoza kikao cha ‘machinjio’

Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anatarajia kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho, cha kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali za mabaraza. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mabaraza hayo ni pamoja na Baraza la Wazee Chadema (Bazecha), Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) na Baraza la Vijana Chadema (Bavicha).

Taarifa iliyotolewa Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema tarehe 6 Desemba 2019, inaeleza kikao hicho kitaketi kwa siku moja (Jumamosi) kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

“Kamati Kuu ya chama itakutana kwa siku moja katika kikao chake cha kikatiba ambapo agenda kuu, itakuwa uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uchaguzi wa mabaraza ya chama. Kikao hicho kitakuwa chini ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mbowe,” inaeleza taarifa ya Makene.

Taarifa hiyo imeeleza zaidi kuwa, baada ya kikao hicho kuketi, Chadema itatoa taarifa kwa umma kuhusu majina ya watakaoteuliwa kuendelea na mchakato wa uchaguzi.

Chadema inatarajia kufanya uchaguzi wa viongozi wake wa kitaifa tarehe 18 Desemba 2019. Ambapo kwa sasa, uchaguzi wa viongozi wa chama hicho wa kanda, umeshafanyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!