ALLY Hapi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema, kazi kubwa zaidi katika uongozi hasa wa kuteuliwa ni kutenda haki. Anaripoti Hamis Mguta, Iringa … (endelea).
Hapi ametoa kauli hiyo leo tarehe 2 Novemba 2019, katika Mkutano wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa kusikiliza kero za wananchi zinazogusa wizara hiyo.
“Waziri, watu hawa ukiwatendea haki kwa kazi unayofanya hii, Mungu anakubariki. Katika nafasi zetu hizi za uongozi, kazi kubwa na ngumu ya kufanya ni kutenda haki.
“Huu ndio mtihani mkubwa wa uongozi hasa sisi viongozi wa kuteuliwa, unakuwaje ni DC ambaye wananchi wako wanalia machozi na kudhulumiwa haki zao? na wewe ukasema mimi ni Mkuu wa Wilaya,” amesema.
“Najua kazi hizi zina changamoto na zina majungu, fitina, zina husda na jinsi pekee ya kujilinda na hayo ni kufanya haki kwa watu wanyonge,” amesema na kuongeza;
“Leo kuna mzee alikuja kunishukuru baada ya kumsaidia mgogoro wake wa kiwanja na akaniambia, amekuja kwa hilo tu na wala hajaja kuomba chochote, mimi nikupongeze unafanya kazi kubwa.”
Leave a comment