Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba wamtema rasmi Aussems, mwenyewe athibitisha
Michezo

Simba wamtema rasmi Aussems, mwenyewe athibitisha

Spread the love

KOCHA wa Simba, Patrick Aussems raia wa Ubelgiji amethibitisha kuvunjwa kwa mkataba wake na klabu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Baada ya kuwepo kwa tetesi za muda mrefu pamoja na vikao vya mara kwa kati nya uongozi wa klabu hiyo na Aussems, hatimaye leo uongozi umempa barua ya kuvunja mkabata.

Aussems alikiri kupokea barua ya kuvunja mkataba wake kwa kuandia kupitia katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa ameitwa na Mkurugenzi wa klabu hiyo na kumpa barua ya kuvunja mkataba wake.

“Mkurugenzi Mkuu na bodi ya Simba, wamenitaarifu kuwa kuanzia sasa mimi sio kocha wa Simba,” aliandika hivyo Aussems.

Miongoni mwa tatizo lililomuondoa kikosi kocha huyo ambaye aliifikisha Simba hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita ni kuondoka nchini bila kufuata taratibu za ruhusa kwa waajiri wake.

Juzi Alhamisi, uongozi wa klabu ya Simba chini ya Mtendaji Mkuu, Senzo Mazingiza uliitisha kikao ambacho Aussems alihudhuria ili kujieleza lakini maswali yote aliyoulizwa ilidaiwa alishindwa kuyatolea ufafanuzi ikiwemo kwanini aliondoka pasipo kufuata utaratibu, alikwenda wapi na kufanya nini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!