Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba wamtema rasmi Aussems, mwenyewe athibitisha
Michezo

Simba wamtema rasmi Aussems, mwenyewe athibitisha

Spread the love

KOCHA wa Simba, Patrick Aussems raia wa Ubelgiji amethibitisha kuvunjwa kwa mkataba wake na klabu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Baada ya kuwepo kwa tetesi za muda mrefu pamoja na vikao vya mara kwa kati nya uongozi wa klabu hiyo na Aussems, hatimaye leo uongozi umempa barua ya kuvunja mkabata.

Aussems alikiri kupokea barua ya kuvunja mkataba wake kwa kuandia kupitia katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa ameitwa na Mkurugenzi wa klabu hiyo na kumpa barua ya kuvunja mkataba wake.

“Mkurugenzi Mkuu na bodi ya Simba, wamenitaarifu kuwa kuanzia sasa mimi sio kocha wa Simba,” aliandika hivyo Aussems.

Miongoni mwa tatizo lililomuondoa kikosi kocha huyo ambaye aliifikisha Simba hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita ni kuondoka nchini bila kufuata taratibu za ruhusa kwa waajiri wake.

Juzi Alhamisi, uongozi wa klabu ya Simba chini ya Mtendaji Mkuu, Senzo Mazingiza uliitisha kikao ambacho Aussems alihudhuria ili kujieleza lakini maswali yote aliyoulizwa ilidaiwa alishindwa kuyatolea ufafanuzi ikiwemo kwanini aliondoka pasipo kufuata utaratibu, alikwenda wapi na kufanya nini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!