TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, wamejitosa katika kinyang’anyiro cha kuwania umakamu mwenyekiti wa chama hicho. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Lissu amechukua na kurejesha fomu ya kugombea umakamu uenyekiti, leo tarehe 30 Novemba 2019, kwa njia ya mtandao, wakati Kubenea akirejesha fomo hiyo katika Ofisi za Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Uchaguzi wa viongozi wa Chadema unatarajiwa kufanyika, tarehe 18 Desemba 2019.
Na leo Jumamosi, ndio mwisho kwa wanachama wa Chadema wanaotaka kugombea nafasi hizo, kurudisha fomu zao kugombea.
Leave a comment