Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mikosi Chadema: Mbowe mgonjwa, wabunge wasota mahabusu
Habari za SiasaTangulizi

Mikosi Chadema: Mbowe mgonjwa, wabunge wasota mahabusu

Mdee, Bulaya, Msigwa na Heche Kisutu
Spread the love

HATIMA ya wabunge wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuendelea kusota lupango au kuwa nje kwa dhamana, wakati wakiendelea kusubiria kesi yao inayowakabili, yaweza kujulikana rasmi kesho, Jumatano. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Wabunge wanaosubiri maamuzi ya mahakama kujua hatima yao ya dhamana, ni Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Halima Mdee (Kawe), John Heche (Tarime Vijijini) na Ester Bulaya (Bunda Mjini).

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, iliamuru kukamatwa kwa wabunge hao, Ijumaa iliyopita, kufuatia kushindwa kufika mahakamani.

Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba alieleza kuwa amefikia maamuzi ya kutoa amri ya kuwakamata Heche, Msigwa, Mdee na Bulaya, baada ya kujiridhisha kuwa wameshindwa kufika mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili na bila mahakama kuelezwa walikokuwa.

Mdee alikamatwa nyumbani kwake Kawe, usiku wa Jumamosi iliyopita; huku Msigwa na Heche, wakikamatwa jana Jumatatu, walipokwenda kwenye Mahakama ya Kisutu kujisalimisha. Bulaya alijisalimisha leo asubuhi.

Wote wanne, wamekabidhiwa kwa jeshi la Polisi kwa ajili ya kuhifadhiwa mpaka kesho, mahakama itakapotoa maamuzi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!