Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mikosi Chadema: Mbowe mgonjwa, wabunge wasota mahabusu
Habari za SiasaTangulizi

Mikosi Chadema: Mbowe mgonjwa, wabunge wasota mahabusu

Mdee, Bulaya, Msigwa na Heche Kisutu
Spread the love

HATIMA ya wabunge wanne wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuendelea kusota lupango au kuwa nje kwa dhamana, wakati wakiendelea kusubiria kesi yao inayowakabili, yaweza kujulikana rasmi kesho, Jumatano. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Wabunge wanaosubiri maamuzi ya mahakama kujua hatima yao ya dhamana, ni Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Halima Mdee (Kawe), John Heche (Tarime Vijijini) na Ester Bulaya (Bunda Mjini).

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, iliamuru kukamatwa kwa wabunge hao, Ijumaa iliyopita, kufuatia kushindwa kufika mahakamani.

Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba alieleza kuwa amefikia maamuzi ya kutoa amri ya kuwakamata Heche, Msigwa, Mdee na Bulaya, baada ya kujiridhisha kuwa wameshindwa kufika mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili na bila mahakama kuelezwa walikokuwa.

Mdee alikamatwa nyumbani kwake Kawe, usiku wa Jumamosi iliyopita; huku Msigwa na Heche, wakikamatwa jana Jumatatu, walipokwenda kwenye Mahakama ya Kisutu kujisalimisha. Bulaya alijisalimisha leo asubuhi.

Wote wanne, wamekabidhiwa kwa jeshi la Polisi kwa ajili ya kuhifadhiwa mpaka kesho, mahakama itakapotoa maamuzi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!