Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi watimiza agizo la Mahakama, Halima Mdee mbaroni
Habari za Siasa

Polisi watimiza agizo la Mahakama, Halima Mdee mbaroni

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe akiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe (Chadema) anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo cha Oysterbay, kwa amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 16 Novemba 2019 na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mdee anashikiliwa baada ya kujisalimisha kituoni hapo.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Mdee alikwenda katika kituo cha polisi cha Oysterbay, kwa ajili ya kumuona Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni (RCO).

Hata hivyo, Polisi wamesema watamshikilia Mdee hadi Jumanne ijayo ya tarehe 19 Novemba 2019, watakapomfikisha mahakamani.

Jana tarehe 15 Novemba 2019 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliamuru Mdee pamoja na wabunge wengine watatu wa Chadema, kukamatwa kutokana na kushindwa kufika mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili, bila ya kutoa taarifa.

Amri hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Thomas Simba.

Wabunge wengine ambao mahakama imeamuru wakamatwe ni Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini, John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini na Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!