Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge kuanza, taarifa ya CAG kuchambuliwa
Habari za Siasa

Bunge kuanza, taarifa ya CAG kuchambuliwa

Bunge la Tanzania
Spread the love

VIKAO vya Kamati 14 za Kudumu za Bunge, vinatarajia kuanza tarehe 21 Oktoba 2019 hadi Novemba Mosi mwaka huu. Anaripoti Hamisi Mguta…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 16 Oktoba 2019 na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa cha Ofisi ya Bunge.

Taarifa hiyo imeleeza kuwa, miongoni mwa shughuli zitakazofanyika katika vikao hivyo, ni uchambuzi wa Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kuhusu hesabu zilizokaguliwa za Serikali za Mitaa na Serikali Kuu.

Pia, Kamati hizo zitafanya uchambuzi wa Taarifa ya Msajili wa Hazina kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma katika mashirika na taasisi mbalimbali nchini.

Na uchambuzi wa Sheria ndogo zilizowasilishwa wakati wa mkutano mkuu wa kumi na sita wa Bunge.Pamoja na Kupokea na kujadili taarifa ya mapendekezo ya mwongozo wa kutayarisha Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!