Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yaongeza siku 3, uandikishaji wapiga kura
Habari za Siasa

Serikali yaongeza siku 3, uandikishaji wapiga kura

Suleiman Jafo, Waziri wa Tamisemi
Spread the love

SERIKALI yaongeza siku tatu katika zoezi la uandikishaji wapiga kura kwenye Daftari la Orodha ya Wapiga Kura. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Zoezi hilo lililoanza tarehe 8 Oktoba 2019 na kutarajiwa kumalizika kesho, sasa litaendelea hadi tarehe 17 Oktoba mwaka huu.

Tangazo hilo limetolewa leo tarehe 13 Oktoba 2019 na Seleman Jaffo, Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Taarifa ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI imeeleza Jafo ametangaza kuongeza siku hizo, ili wananchi wapate fursa ya kujiandikisha.

“Waziri Jafo atangaza kuongeza siku Tatu za Uandikishaji wa Wapiga kura kwenye Daftari la Orodha ya Wapiga Kura; Sasa zoezi hilo litakamilika Tarehe 17/10/2019,” imeeleza taarifa hiyo.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!