Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto akwama, mahakama yakwama
Habari za Siasa

Zitto akwama, mahakama yakwama

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo tarehe 7 Oktoba 2019, imekwama kuendelea na kesi ya uchochezi inayomkabili Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini kwa madai ya kufiwa. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Peter Kibatala, Wakili wa Utetezi amemweleza Hakimu Mkazi mkuu, Huruma Shaidi kwamba mteja wake (Zitto), amefiwa mkoani Kigoma hivyo ameshindwa kufika mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilikuwa imefika mbele ya Hakimu Huruma kwa ajili ya kusikilizwa. Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo anakabiliwa na kesi ya uchochezi, anadai wa kutenda makossa hayo tarehe 28 Oktoba 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Nassoro Katuga, wakili wa serikali mbele ya Hakimu Shaidi alisema, shauri hilo lilikuwa limefikishwa kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa ambapo tayari mashahidi wane wametoa ushahidi wao.

Hakimu Huruma amepanga kuendelea kusikiza shuri hilo tarehe 22, 23 Oktoba 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!