Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto akwama, mahakama yakwama
Habari za Siasa

Zitto akwama, mahakama yakwama

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo tarehe 7 Oktoba 2019, imekwama kuendelea na kesi ya uchochezi inayomkabili Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini kwa madai ya kufiwa. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Peter Kibatala, Wakili wa Utetezi amemweleza Hakimu Mkazi mkuu, Huruma Shaidi kwamba mteja wake (Zitto), amefiwa mkoani Kigoma hivyo ameshindwa kufika mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilikuwa imefika mbele ya Hakimu Huruma kwa ajili ya kusikilizwa. Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo anakabiliwa na kesi ya uchochezi, anadai wa kutenda makossa hayo tarehe 28 Oktoba 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

Nassoro Katuga, wakili wa serikali mbele ya Hakimu Shaidi alisema, shauri hilo lilikuwa limefikishwa kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa ambapo tayari mashahidi wane wametoa ushahidi wao.

Hakimu Huruma amepanga kuendelea kusikiza shuri hilo tarehe 22, 23 Oktoba 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!