Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Ruwai’chi atolewa ICU
Habari Mchanganyiko

Askofu Ruwai’chi atolewa ICU

Spread the love

MHASHAMU Yuda Thadeus Ruwai’chi, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam, ametolewa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kiongozi huyo wa kiroho mepelekwa katika wodi ya kawaida, baada ya hali yake kiafya kuanza kuimarika.

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 16 Septemba 2019, na Kitengo cha Uhusiano cha Taasisi ya mifupa (MOI).

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, jopo la wataalamu saba wanaomhudumia Askofu Ruwai’chi limemamua kumhamisha kutoka ICU kwenda wodi za kawaida, baada ya kujiridhisha na maendeleo ya afya yake.

Taarifa hiyo inaeleza kwamba, awali jopo hilo la wataalamu lilifanya tathimini ya vipimo pamoja na taarifa mbalimbali za maendeleo ya Askofu Ruwai’chi tangu alivyopokelewa na kufanyiwa upasuaji MOI tarehe 9 Septemba 2019.

“Taasisi ya MOI inawahakikishia Watanzania wote hususan waumini wa Kanisa Katoliki kwamba Askofu Ruwai’chi yuko salama na afya yake imeimarika sana hivyo waendelee kumuombea ili arejee kwenye majukumu yake,” inaeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!